Biblia inasema nini kuhusu Adulamu – Mistari yote ya Biblia kuhusu Adulamu

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Adulamu

1 Samweli 22 : 1
1 Basi Daudi akaondoka huko, akakimbilia pango la Adulamu; na ndugu zake na watu wote wa ukoo wa baba yake waliposikia habari hiyo, wakamwendea huko.

2 Samweli 23 : 13
13 Tena, watatu miongoni mwa wale thelathini waliokuwa wakuu wakashuka, wakamwendea Daudi wakati wa mavuno mpaka pango la Adulamu, na kikosi cha Wafilisti walikuwa wamefanya kambi katika bonde la Warefai.

1 Mambo ya Nyakati 11 : 15
15 ⑫ Tena, watatu miongoni mwa wale thelathini waliokuwa wakuu wakashuka mwambani, wakamwendea Daudi, hadi pango la Adulamu; na jeshi la Wafilisti walikuwa wamefanya kambi bondeni mwa Warefai.

Zaburi 57 : 11
11 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, Na juu ya nchi yote uwe utukufu wako.

Zaburi 142 : 7
7 Uitoe nafsi yangu kifungoni. Nipate kulishukuru jina lako. Wenye haki watanizunguka, Kwa kuwa Wewe unanikirimu.

Mwanzo 38 : 1
1 ⑳ Ikawa wakati ule, Yuda akashuka kutoka kwa ndugu zake, akamfikia mtu Mwadulami, jina lake Hira.

Yoshua 12 : 15
15 mfalme wa Libna, mmoja; na mfalme wa Adulamu, mmoja;

Yoshua 15 : 35
35 Yarmuthi, Adulamu, Soko, Azeka;

2 Mambo ya Nyakati 11 : 7
7 Beth-suri, Soko, Adulamu,

Nehemia 11 : 30
30 Zanoa, Adulamu na vijiji vyake, Lakishi na mashamba yake, Azeka na vijiji vyake. Hivyo wakakaa toka Beer-sheba mpaka bonde la Hinomu.

Mika 1 : 15
15 Bado, wakazi wa Maresha, nitawaleteeni tena yeye atakayewamiliki; Utukufu wa Israeli utafika Adulamu.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *