Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Tumbo
Ayubu 15 : 2
2 Je! Yapasa mtu mwenye hekima kujibu kwa ujuzi wa uvuvio, Na kulijaza tumbo lake upepo wa mashariki?
Ayubu 15 : 35
35 Wao hutunga mimba ya madhara, na kuzaa uovu, Na mioyo yao hutunga udanganyifu.
Ayubu 20 : 20
20 ⑮ Kwa sababu hakujua utulivu ndani yake, Hataokoa chochote kutoka hicho alichokifurahia.
Zaburi 44 : 25
25 Maana nafsi yetu imeinama mavumbini, Tumbo letu limegandamana na nchi.
Mithali 18 : 20
20 Tumbo la mtu litajazwa matunda ya kinywa chake; Atashiba mazao ya midomo yake.
Mithali 20 : 27
27 Pumzi ya mwanadamu ni taa ya BWANA; Hupeleleza yote yaliyomo ndani yake.
Mithali 20 : 30
30 Machubuko ya fimbo husafisha uovu, Na mapigo hufikia ndani ya mtima.
Habakuki 3 : 16
16 Nikasikia, na tumbo langu likatetemeka, Midomo yangu ikatikisika kwa sauti ile; Ubovu ukaingia mifupani mwangu, Nikatetemeka katika mahali pangu; Ili nipate kuingoja ile siku ya dhiki, Kundi lao washambuliao wakweapo juu ya watu.
Yohana 7 : 38
38 Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake.
Tito 1 : 12
12 Mmoja wao, nabii wao wenyewe, amesema, Wakrete ni waongo siku zote, wanyama wabaya, walafi wavivu.
Leave a Reply