Biblia inasema nini kuhusu Tafsiri – Mistari yote ya Biblia kuhusu Tafsiri

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Tafsiri

Mwanzo 5 : 24
24 Henoko akaenda pamoja na Mungu, naye akatoweka, maana Mungu alimtwaa.

Waraka kwa Waebrania 11 : 5
5 Kwa imani Henoko alihamishwa, asije akaona mauti, wala hakuonekana, kwa sababu Mungu alimhamisha; maana kabla ya kuhamishwa alikuwa ameshuhudiwa kwamba amempendeza Mungu.

2 Wafalme 2 : 12
12 Naye Elisha akaona, akalia, Baba yangu, baba yangu, gari la Israeli na wapanda farasi wake! Asimwone tena kabisa; akashika mavazi yake mwenyewe, akayararua vipande viwili.

Marko 16 : 19
19 ⑤ Basi Bwana Yesu, baada ya kusema nao, akachukuliwa juu mbinguni, akaketi mkono wa kulia wa Mungu.

Luka 24 : 51
51 Ikawa katika kuwabariki, alijitenga nao; akachukuliwa juu mbinguni.

Matendo 1 : 11
11 wakasema, Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni.

2 Wakorintho 5 : 4
4 Kwa sababu sisi tulio katika maskani hii twapumua kwa shida, tukilemewa; si kwamba twataka kuvuliwa, bali kuvikwa, ili kitu kile kipatikanacho na mauti kimezwe na uzima.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *