Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Tafsiri
Mwanzo 5 : 24
24 Henoko akaenda pamoja na Mungu, naye akatoweka, maana Mungu alimtwaa.
Waraka kwa Waebrania 11 : 5
5 Kwa imani Henoko alihamishwa, asije akaona mauti, wala hakuonekana, kwa sababu Mungu alimhamisha; maana kabla ya kuhamishwa alikuwa ameshuhudiwa kwamba amempendeza Mungu.
2 Wafalme 2 : 12
12 Naye Elisha akaona, akalia, Baba yangu, baba yangu, gari la Israeli na wapanda farasi wake! Asimwone tena kabisa; akashika mavazi yake mwenyewe, akayararua vipande viwili.
Marko 16 : 19
19 ⑤ Basi Bwana Yesu, baada ya kusema nao, akachukuliwa juu mbinguni, akaketi mkono wa kulia wa Mungu.
Luka 24 : 51
51 Ikawa katika kuwabariki, alijitenga nao; akachukuliwa juu mbinguni.
Matendo 1 : 11
11 wakasema, Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni.
2 Wakorintho 5 : 4
4 Kwa sababu sisi tulio katika maskani hii twapumua kwa shida, tukilemewa; si kwamba twataka kuvuliwa, bali kuvikwa, ili kitu kile kipatikanacho na mauti kimezwe na uzima.
Leave a Reply