Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Nzuri kwa Ubaya
Mathayo 5 : 48
48 Basi ninyi iweni wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.
Luka 6 : 36
36 Basi, iweni na huruma, kama Baba yenu alivyo na huruma.
Mwanzo 20 : 18
18 Maana BWANA alikuwa ameyafunga matumbo ya watu wa nyumbani mwa Abimeleki, wasizae, kwa ajili ya Sara mkewe Abrahamu.
1 Samweli 24 : 17
17 Akamwambia Daudi, Wewe u mwenye haki kuliko mimi; maana wewe umenitendea mema, nami nimekutenda mabaya.
2 Wafalme 6 : 23
23 Basi akawaandalia chakula tele; nao walipokwisha kula na kunywa, akawaacha, wakaenda zao kwa bwana wao. Na vikosi vya Shamu havikuja tena katika nchi ya Israeli.
Zaburi 35 : 14
14 Nilisikitika kana kwamba ni rafiki au ndugu yangu, Niliinama nikilia kama aliyefiwa na mamaye.
Luka 23 : 34
34 ③ Yesu akasema, Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. Wakagawa mavazi yake, wakipiga kura.
Leave a Reply