Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia muziki katika ibada
Zaburi 95 : 1
1 Njoni, tumwimbie BWANA, Tumfanyie shangwe mwamba wa wokovu wetu.
Zaburi 150 : 1 – 6
1 Haleluya. Msifuni Mungu katika patakatifu pake; Msifuni katika anga la uweza wake.
2 Msifuni kwa matendo yake makuu; Msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.
3 Msifuni kwa mvumo wa baragumu; Msifuni kwa kinanda na kinubi;
4 Msifuni kwa matari na kucheza; Msifuni kwa zeze na filimbi;
5 Msifuni kwa matoazi yaliayo; Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.
6 ① Kila mwenye pumzi na amsifu BWANA. Haleluya.
Wakolosai 3 : 16
16 Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.
Waefeso 5 : 19
19 mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu;
Matendo 16 : 25
25 Lakini ilipokuwa karibu usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza.
Zaburi 100 : 1 – 2
1 Mshangilieni BWANA, enyi nchi zote;
2 Mtumikieni BWANA kwa furaha; Njoni mbele zake mkiimba;
Zaburi 71 : 23
23 ⑮ Midomo yangu itafurahi sana nikuimbiapo, Na nafsi yangu uliyoikomboa.
Yakobo 5 : 13
13 Kuna mtu miongoni mwenu anayeteseka? Na aombe. Ana moyo wa kuchangamka? Na aimbe zaburi.
Warumi 15 : 9
9 tena ili Mataifa wamtukuze Mungu kwa ajili ya rehema zake; kama ilivyoandikwa, Kwa hiyo nitakushukuru kati ya Mataifa, Nami nitaliimbia jina lako.
Zaburi 33 : 3
3 Mwimbieni wimbo mpya, Pigeni kwa ustadi kwa sauti ya shangwe.
Zaburi 149 : 3
3 Na walisifu jina lake kwa kucheza, Kwa sauti tamu ya matari na kinubi.
Waefeso 5 : 18 – 20
18 Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;
19 mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu;
20 na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo.
Mathayo 26 : 30
30 ⑥ Nao walipokwisha kuimba, wakatoka nje kwenda katika mlima wa Mizeituni.
Waraka kwa Waebrania 2 : 12
12 akisema, Nitalihubiri jina lako kwa ndugu zangu; Katikati ya kanisa nitakuimbia sifa.
Yohana 4 : 24
24 Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.
Zaburi 150 : 4
4 Msifuni kwa matari na kucheza; Msifuni kwa zeze na filimbi;
Zaburi 9 : 2
2 Nitafurahi na kukushangilia; Nitaliimbia sifa jina lako, Wewe Uliye juu.
2 Samweli 6 : 5
5 Daudi na nyumba yote ya Israeli wakacheza mbele za BWANA kwa nguvu zao zote, kwa nyimbo, na kwa vinubi, na kwa vinanda, na kwa matari, na kwa kayamba, na kwa matoazi.
2 Samweli 6 : 14
14 ⑲ Daudi akacheza mbele za BWANA kwa nguvu zake zote; na Daudi alikuwa amevaa naivera ya kitani.
Wafilipi 4 : 8
8 Hatimaye, ndugu zangu, mambo yoyote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo ya heshima, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote yenye kupendeza, yoyote yenye sifa njema; ukiwapo wema wowote, ikiwapo sifa nzuri yoyote, yatafakarini hayo.
Leave a Reply