Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Mtangazaji
Mambo ya Walawi 19 : 16
16 ⑳ Usiende huku na huko katikati ya watu wako, kama mchongezi; wala usijifaidi kwa damu[9] ya jirani yako; mimi ndimi BWANA.
Zaburi 15 : 3
3 Asiyesingizia kwa ulimi wake. Wala kumtenda mwenziwe mabaya, Wala kumsengenya jirani yake.
Mithali 11 : 13
13 Mwenye udaku hupitapita akifunua siri; Bali mwenye roho ya uaminifu husitiri mambo.
Mithali 16 : 28
28 Mtu mshupavu huleta fitina; Na mchongezi huwafarakanisha rafiki.
Mithali 17 : 9
9 Afunikaye kosa hutafuta kupendwa; Bali yeye afichuaye siri hutenga rafiki.
Mithali 18 : 8
8 Maneno ya mchongezi ni kama vitoweo; Nayo hushukia pande za ndani za tumbo.
Mithali 20 : 19
19 Mwenye udaku hufunua siri; Basi, usishirikiane naye afunuaye midomo yake sana.
Mithali 26 : 22
22 Maneno ya mchongezi ni kama vitoweo. Nayo hushukia pande za ndani za tumbo.
1 Timotheo 5 : 11
11 Bali wajane walio vijana ukatae kuwaandika hao, maana, wakizidiwa na tamaa kinyume cha Kristo, wataka kuolewa;
Mwanzo 37 : 2
2 Hivi ndivyo vizazi vya Yakobo. Yusufu, aliyekuwa mwenye miaka kumi na saba, alikuwa akichunga kondoo pamoja na ndugu zake; naye alikuwa kijana pamoja na wana wa Bilha, na wana wa Zilpa, wake wa baba yake. Yusufu akamletea baba yao habari zao mbaya.
2 Samweli 3 : 23
23 Hata Yoabu, na jeshi lote waliokuwa pamoja naye, walipofika, watu wakamwambia Yoabu, wakisema, Abneri, mwana wa Neri, alikuja kwa mfalme, naye amemruhusu, naye amekwenda zake kwa amani.
Leave a Reply