Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia milima
Zaburi 95 : 4 – 5
4 Mkononi mwake zimo bonde za dunia, Hata vilele vya milima ni vyake.
5 Bahari ni yake, ndiye aliyeifanya, Na mikono yake iliumba nchi kavu.
Zaburi 104 : 5 – 9
5 Uliiweka nchi juu ya misingi yake, Isitikisike milele.
6 Uliifunika kwa vilindi kama kwa vazi, Maji yalikuwa yakisimama juu ya milima.
7 Kwa kukemea kwako yakakimbia, Kwa sauti ya radi yako yakaenda zake kasi,
8 ⑲ Yakapanda milima, yakateremka mabondeni, Mpaka mahali ulipoyatengenezea.
9 ⑳ Umeweka mpaka yasiupite, Wala yasirudi kuifunikiza nchi.
Leave a Reply