Biblia inasema nini kuhusu Mikali – Mistari yote ya Biblia kuhusu Mikali

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Mikali

1 Samweli 18 : 28
28 Sauli akaona na kutambua ya kwamba BWANA alikuwa pamoja na Daudi; na huyo Mikali, binti Sauli, akampenda.

1 Samweli 19 : 17
17 ⑤ Sauli akamwambia Mikali, Mbona wewe umenidanganya hivi, na kumwacha adui yangu aende, hata ameniponyoka? Naye Mikali akamjibu Sauli, Yeye aliniambia, Niache niende zangu; kwa nini nikuue?

1 Samweli 25 : 44
44 ⑲ Lakini Sauli alikuwa amemposa Mikali, binti yake aliyekuwa mkewe Daudi, kwa Palti, mwana wa Laisha aliyekuwa mtu wa Galimu.

2 Samweli 3 : 16
16 Huyo mumewe akafuatana naye, huku akilia, akamfuata mpaka Bahurimu. Ndipo Abneri akamwambia, Haya, rudi. Naye akarudi.

2 Samweli 6 : 16
16 Ikawa, sanduku la BWANA lilipoingia mji wa Daudi, Mikali binti Sauli, akachungulia dirishani, akamwona mfalme Daudi akirukaruka na kucheza mbele za BWANA; akamdharau moyoni mwake.

2 Samweli 6 : 23
23 Basi Mikali, binti Sauli, hakuwa na mtoto hata siku ya kufa kwake.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *