Biblia inasema nini kuhusu Kuweka maiti – Mistari yote ya Biblia kuhusu Kuweka maiti

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Kuweka maiti

Mwanzo 50 : 3
3 ⑩ Siku zake arubaini zikaisha, maana siku hizo zilitimiza siku za wale waliohifadhiwa kwa kupakwa dawa. Wamisri wakamwombolezea siku sabini.

Mwanzo 50 : 26
26 Basi Yusufu akafa, mwenye miaka mia moja na kumi; wakampaka dawa, wakamtia katika sanduku, huko Misri.

2 Mambo ya Nyakati 16 : 14
14 ② Wakamzika katika makaburi yake mwenyewe, aliyojichimbia katika mji wa Daudi, wakamlaza juu ya kitanda kilichojazwa manukato, na kila namna ya machanganyiko ya hao mafundi wa dawa; wakawasha moto mkubwa sana kwa heshima yake.

Marko 15 : 46
46 Naye akanunua sanda ya kitani, akamteremsha, akamfungia ile sanda, akamweka katika kaburi lililochongwa mwambani; akavingirisha jiwe mbele ya mlango wa kaburi.

Marko 16 : 1
1 Na sabato ilipokwisha kupita, Mariamu Magdalene na Mariamu mamaye Yakobo, na Salome walinunua manukato wapate kwenda kumpaka.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *