Biblia inasema nini kuhusu kuthaminiana – Mistari yote ya Biblia kuhusu kuthaminiana

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia kuthaminiana

Yohana 13 : 34 – 35
34 Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.
35 Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.

1 Yohana 4 : 8
8 Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo.

Yohana 15 : 13
13 Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.

2 Wakorintho 10 : 5
5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo;

Waefeso 4 : 32
32 ⑱ tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.

1 Yohana 4 : 19
19 Sisi tunapenda kwa maana yeye alitupenda sisi kwanza.

Yohana 15 : 3
3 Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililowaambia.

Marko 9 : 7
7 ⑳ Kisha likatokea wingu, likawatia uvuli; sauti ikatoka katika lile wingu, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, msikieni yeye.

Mathayo 24 : 45 – 51
45 Ni nani basi yule mtumwa mwaminifu mwenye akili, ambaye bwana wake alimweka juu ya nyumba yake, awape watu chakula kwa wakati wake?
46 Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta akifanya hivyo.
47 ⑬ Amin, nawaambieni, atamweka juu ya vitu vyake vyote.
48 ⑭ Lakini mtumwa yule mbaya akisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia;
49 akaanza kuwapiga watumwa wenzake, na kula na kunywa pamoja na walevi;
50 bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyotazamia, na saa asiyojua,
51 ⑮ atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wanafiki; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.

Yohana 15 : 5
5 Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamuwezi kufanya neno lolote.

Matendo 16 : 31
31 Wakamwambia, Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako.

1 Petro 3 : 15
15 Muwe tayari siku zote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa heshima.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *