Biblia inasema nini kuhusu kusaidia wengine – Mistari yote ya Biblia kuhusu kusaidia wengine

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia kusaidia wengine

2 Wathesalonike 3 : 13
13 ⑧ Lakini ninyi, ndugu, msikate tamaa katika kutenda mema.

Luka 6 : 38
38 Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwasukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa.

Yakobo 1 : 27
27 Dini iliyo safi, isiyo na dosari mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.

Yakobo 2 : 8
8 Lakini mkiitimiza ile sheria ya kifalme kama ilivyoandikwa, Mpende jirani yako kama nafsi yako, mwatenda vema.

1 Petro 5 : 3
3 ⑭ Wala si kama wajifanyao mabwana wa wale walio chini ya utunzaji wao, bali iweni mifano kwa lile kundi.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *