Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Kiwavi
1 Wafalme 8 : 37
37 Ikiwa kuna njaa katika nchi, au tauni, au ukosefu wa mvua, au ukungu, au nzige, au panzi; ikiwa adui wamewazingira katika mji wao wowote ule;[17] au ukiwapo msiba wowote, au ugonjwa wowote;
Zaburi 78 : 46
46 ③ Akawapa tunutu mazao yao, Na nzige matunda ya kazi yao.
Zaburi 105 : 34
34 ⑮ Alisema, kukaja nzige, Na tunutu wasiohesabika;
Yeremia 51 : 27
27 ⑲ Itwekeni bendera katika nchi, pigeni tarumbeta kati ya mataifa, yawekeni mataifa tayari juu yake; ziiteni juu yake falme za Ararati, na Mini, na Ashkenazi; agizeni jemadari juu yake; wapandisheni farasi, kama tunutu.
Yoeli 1 : 4
4 Yaliyosazwa na tunutu yameliwa na nzige; na yaliyosazwa na nzige yameliwa na parare; na yaliyosazwa na parare yameliwa na madumadu.
Yoeli 2 : 25
25 Nami nitawarudishia hiyo miaka iliyoliwa na nzige, na parare, na madumadu, na tunutu, jeshi langu kubwa nililotuma kati yenu.
Leave a Reply