KUWA HAZINA YA MUNGU

Kumb.26.18 Na leo MUNGU amethibitisha tena ya kuwa ninyi mmetunzwa, kama alivyoahidi, watu waliokabidhiwa kuzishika amri zake, (MSB) *WENYE KUWEKA HAZINA YA MUNGU* ninaamini sana ya kwamba andiko hili halikuandikiwa wateule wachache. lakini kwa kila mwamini,,,sisi ni taifa la kipekee unajua Mungu ametuthamini sana kuliko kitu kingine ndiyo maana hakutuumba kwa mfano wa mnyama. lakini kwa sura yake mwenyewe maana yake hamna kitu cha maana Kama wewe ni mtoto wa Mungu kwahiyo kumbuka kila siku kuwa Mungu wako anahusika na kila jambo linalokuhusu Halleluyah,, Ametuamini sana kwa mambo haya. ,,umekumbushwa juu ya andiko hili “Mathayo 6:21” hazina yako ilipo,, ndipo moyo wako utakapokuwa,, kumaanisha ukweli kwamba Mungu ametuthamini, huwa anatuwazia kila mmoja wetu. siku,, kila kitu kizuri anatuwazia kwa sababu anatuambia kuwa ana mipango mizuri kwetu maana akikuona, anajiona vyake kabisa. Wapendwa jambo moja ninaloweza kutuhakikishia ni kwamba hata tunapohisi kulemewa na hali ya ulimwengu wetu, tunaweza angalau kusimama pamoja na vizazi vilivyomtumaini Mungu kwa subira kwa sababu tuna hakika atalitimiza neno lake. *SOMO ZAIDI* Mathayo 6:21 Kumbukumbu la Torati 32:9 *NUKUU* Jikumbushe wewe mtoto wa Mungu kila siku nyingine kwamba Mungu wako anajishughulisha na kila jambo linalokuhusu na kumwazia Mungu juu yako. *SALA:* Baba katika jina la Yesu, tunakushukuru kwa neno lako linalotuonyesha jinsi unavyotujali, tunaelewa jinsi unavyotuwazia kwa sababu umetuthamini, tunachagua kuhama kama wateule. wa Mungu na uangalie neno lako katika jina la Yesu tumeomba .AMEN

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *