Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia jinsi ya kumngoja Mungu
Zaburi 27 : 13 – 14
13 ① Naamini ya kuwa nitauona wema wa BWANA Katika nchi ya walio hai.
14 ② Umtumainie BWANA, uwe imara, Upige moyo konde, naam, umngoje BWANA.
Wafilipi 1 : 6
6 Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu;
Yakobo 1 : 2 – 3
2 Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali;
3 mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi.
Yohana 8 : 32
32 tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.
1 Wathesalonike 5 : 16 – 18
16 Furahini siku zote;
17 ombeni bila kukoma;
18 shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.
Maombolezo 3 : 21 – 23
21 Najikumbusha neno hili, Kwa hiyo nina matumaini.
22 Ni huruma za BWANA kwamba hatuangamii, Kwa kuwa rehema zake hazikomi.
23 Ni mpya kila siku asubuhi; Uaminifu wako ni mkuu.
Leave a Reply