Biblia inasema nini kuhusu wakati wa mavuno – Mistari yote ya Biblia kuhusu wakati wa mavuno

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia wakati wa mavuno

Luka 10 : 2
2 Akawaambia, Mavuno ni mengi, lakini wafanya kazi ni wachache; basi mwombeni Bwana wa mavuno apeleke wafanya kazi katika mavuno yake.

Yohana 4 : 35
35 Hamsemi ninyi, Bado miezi minne, ndipo yanakuja mavuno? Tazama, mimi nawaambieni, Inueni macho yenu myatazame mashamba, ya kuwa yamekwisha kuwa meupe, tayari kwa mavuno.

Mathayo 13 : 30
30 Viacheni vyote vikue hadi wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni mkaiweke ghalani mwangu.

Mathayo 9 : 37
37 Ndipo alipowaambia wanafunzi wake, Mavuno ni mengi, lakini wafanya kazi ni wachache.

Yakobo 5 : 7
7 Kwa hiyo ndugu, vumilieni, hata kuja kwake Bwana. Tazama, mkulima hungoja mazao ya nchi yaliyo ya thamani, huvumilia kwa ajili yake hata yatakapopata mvua ya kwanza na ya mwisho.

Mithali 3 : 9
9 ⑥ Mheshimu BWANA kwa mali yako, Na kwa malimbuko ya mazao yako yote.

Mathayo 13 : 37 – 43
37 Akajibu, akasema, Azipandaye zile mbegu njema ni Mwana wa Adamu;
38 ② lile shamba ni ulimwengu; zile mbegu njema ni wana wa ufalme; na yale magugu ni wana wa yule mwovu;
39 yule adui aliyeyapanda ni Ibilisi; mavuno ni mwisho wa dunia; na wale wavunao ni malaika.
40 ③ Basi, kama vile magugu yakusanywavyo na kuchomwa motoni; ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia.
41 ④ Mwana wa Adamu atawatuma malaika wake, nao watakusanya kutoka katika ufalme wake machukizo yote, na hao watendao maasi,
42 ⑤ na kuwatupa katika tanuri ya moto, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
43 ⑥ Ndipo wenye haki watakapong’aa kama jua katika ufalme wa Baba yao. Mwenye masikio, na asikie.

Mathayo 9 : 37 – 38
37 Ndipo alipowaambia wanafunzi wake, Mavuno ni mengi, lakini wafanya kazi ni wachache.
38 Basi mwombeni Bwana wa mavuno, atume wafanya kazi katika mavuno yake.

Zaburi 100 : 1 – 5
1 Mshangilieni BWANA, enyi nchi zote;
2 Mtumikieni BWANA kwa furaha; Njoni mbele zake mkiimba;
3 Jueni kwamba BWANA ndiye Mungu; Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake; Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake.
4 Ingieni malangoni mwake kwa shukrani; Nyuani mwake kwa kusifu; Mshukuruni, lihimidini jina lake;
5 Maana BWANA ni mwema; Rehema zake ni za milele; Na uaminifu wake katika vizazi vyote.

Wagalatia 6 : 9
9 Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho.

Luka 8 : 11
11 Na huo mfano, maana yake ni hii; Mbegu ni neno la Mungu.

Ufunuo 14 : 14 – 16
14 Kisha nikaona, na tazama, wingu jeupe, na juu ya wingu hilo ameketi mmoja, mfano wa Mwanadamu, mwenye taji la dhahabu juu ya kichwa chake, na katika mkono wake mundu mkali.
15 Na malaika mwingine akatoka katika hekalu, akimlilia kwa sauti kuu yeye aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu, Tia mundu wako, ukavune; kwa kuwa saa ya kuvuna imekuja; kwa kuwa mavuno ya nchi yamekomaa.
16 Na yeye aliyeketi juu ya wingu akautupa mundu wake juu ya nchi, nchi ikavunwa.

Yeremia 8 : 20
20 Mavuno yamepita, wakati wa joto umekwisha, wala sisi hatukuokoka.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *