Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia wajibu wa mzazi
Mithali 22 : 6
6 Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.
Waefeso 6 : 4
4 ② Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maagizo ya Bwana.
Kumbukumbu la Torati 6 : 7
7 nawe uwafundishe watoto wako kwa bidii, na kuyasema uishipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo.
Kumbukumbu la Torati 6 : 6 – 7
6 Na maneno haya ninayokuamuru leo, yatakuwa katika moyo wako;
7 nawe uwafundishe watoto wako kwa bidii, na kuyasema uishipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo.
Wakolosai 3 : 21
21 Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, wasije wakakata tamaa.
Leave a Reply