Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Uzito
Mambo ya Walawi 19 : 36
36 Mizani ya haki, vipimo vya haki, efa ya haki, hini ya haki, ndivyo mtakavyokuwa navyo. Mimi ndimi BWANA, Mungu wenu, niliyewatoa katika nchi ya Misri.
Kumbukumbu la Torati 25 : 15
15 Uwe na jiwe timilifu la haki, uwe na kipimo kitimilifu cha haki; zipate kuwa nyingi siku zako, katika nchi akupayo BWANA, Mungu wako.
Mithali 11 : 1
1 Mizani ya udanganyifu ni chukizo kwa BWANA; Bali vipimo vilivyo sawasawa humpendeza.
Mithali 16 : 11
11 ⑭ Mizani ya haki na vitanga vyake ni vya BWANA; Mawe yote ya mfukoni ni kazi yake.
Mithali 20 : 10
10 Vipimo mbalimbali, na pishi mbalimbali, Vyote viwili ni chukizo kwa BWANA.
Mithali 20 : 23
23 Vipimo mbalimbali ni chukizo kwa BWANA; Tena mizani ya hila si njema.
Leave a Reply