Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia uvumi
Kutoka 23 : 1
1 Usivumishe habari za uongo; usishirikiane na mwovu kwa kuwa shahidi wa uongo.
Mithali 11 : 13 – 14
13 Mwenye udaku hupitapita akifunua siri; Bali mwenye roho ya uaminifu husitiri mambo.
14 Pasipo mashauri taifa huanguka; Bali kwa wingi wa washauri huja wokovu.
Yakobo 4 : 1 – 2
1 Vita vyatoka wapi, na mapigano yaliyoko kati yenu yatoka wapi? Si humu, katika tamaa zenu zifanyazo vita katika viungo vyenu?
2 Mwatamani, wala hamna kitu, mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi!
Mithali 26 : 20
20 Moto hufa kwa kukosa kuni; Na bila mchongezi fitina hukoma.
Mithali 21 : 15
15 Ni furaha yao wenye haki kutenda hukumu; Lakini ni uharibifu kwao watendao maovu.
Mathayo 7 : 12
12 ⑰ Basi yoyote myatakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo; maana hiyo ndiyo Torati na Manabii.
Leave a Reply