Biblia inasema nini kuhusu Uvivu – Mistari yote ya Biblia kuhusu Uvivu

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Uvivu

Mithali 6 : 6
6 Ewe mvivu, mwendee chungu, Zitafakari njia zake ukapate hekima.

Mithali 6 : 11
11 Hivyo umaskini wako huja kama mnyang’anyi, Na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha.

Mithali 10 : 5
5 Akusanyaye wakati wa joto ni mwana mwenye hekima; Bali asinziaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.

Mithali 10 : 26
26 Kama siki menoni, na kama moshi machoni, Ndivyo alivyo mtu mvivu kwa hao waliomwajiri.

Mithali 12 : 9
9 Afadhali mtu anayedharauliwa, ikiwa ana mtumwa, Kuliko ajisifuye, ikiwa anahitaji chakula.

Mithali 12 : 24
24 ⑥ Mkono wa mwenye bidii utatawala; Bali mvivu atalipishwa kodi.

Mithali 12 : 27
27 Mtu mvivu hapiki mawindo yake; Bali mwenye bidii anazo mali za thamani.

Mithali 13 : 4
4 Nafsi ya mtu mvivu hutamani asipate kitu; Bali nafsi ya mwenye bidii itanenepeshwa.

Mithali 14 : 23
23 Katika kila kazi mna faida; Bali maneno ya midomo huleta hasara tu.

Mithali 15 : 19
19 Njia ya mtu mvivu ni kama boma la miiba; Bali mapito yao wenye unyofu hufanyika njia kuu.

Mithali 18 : 9
9 Yeye naye aliye mvivu katika kazi yake, Ni ndugu yake aliye mharibifu.

Mithali 19 : 15
15 Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito; Na nafsi yake mvivu itaona njaa.

Mithali 19 : 24
24 Mtu mvivu hutia mkono wake katika sahani; Wala hataki hata kuupeleka kinywani pake.

Mithali 20 : 4
4 Mtu mvivu hataki kulima wakati wa baridi; Hivyo wakati wa mavuno ataomba, hana kitu.

Mithali 20 : 13
13 ⑩ Usipende usingizi usije ukawa maskini; Fumbua macho yako nawe utashiba chakula.

Mithali 21 : 25
25 Matakwa yake mtu mvivu humwua, Kwa maana mikono yake hukataa kufanya kazi.

Mithali 23 : 21
21 Kwa maana mlevi na mlafi huingia umaskini, Na utepetevu humvika mtu nguo mbovu.

Mithali 24 : 31
31 ⑧ Kumbe! Lote pia limemea miiba; Uso wake ulifunikwa kwa viwawi; Na ukuta wake wa mawe umebomoka.

Mithali 24 : 34
34 Hivyo, umaskini wako huja kama mnyang’anyi, Na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha.

Mithali 26 : 16
16 Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake, Kuliko watu saba wawezao kutoa sababu.

Mithali 22 : 13
13 Mtu mvivu husema, Simba yuko nje; Nitauawa katika njia kuu.

Mhubiri 4 : 5
5 Mpumbavu huikunja mikono yake, Naye hula chakula chake mwenyewe;

Mhubiri 10 : 18
18 Kwa sababu ya uvivu paa hunepa; Na kwa ulegevu wa mikono nyumba huvuja.

Isaya 56 : 10
10 Walinzi wake ni vipofu, wote pia hawana maarifa; wote ni mbwa walio bubu, hawawezi kulia; huota ndoto, hulala, hupenda usingizi.

Ezekieli 16 : 49
49 ⑮ Tazama, uovu wa dada yako, Sodoma, ulikuwa huu; kiburi, na kushiba chakula, na kufanikiwa, hayo yalikuwa ndani yake na binti zake; lakini hukuwasaidia maskini na wahitaji.

Luka 19 : 25
25 Wakamwambia, Bwana, anayo mafungu kumi.

Mathayo 20 : 7
7 Wakamwambia, Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Akawaambia, nanyi pia nendeni katika shamba la mizabibu.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *